Wednesday, December 16, 2009

MAZOEZI


Timu ya Shein Rangers Sports Club inaendelea na mazoezi yake ya kawaida kila siku katika uwanja wa TP Sinza.

Monday, December 14, 2009

AZAM BINGWA TENA


Timu ya Azam United chini ya miaka 20 imeichapa Simba Sports Club chini ya miaka 20 bao 3 - 1 na kuwa mabingwa wa UHAI CUP kwa mwaka wa pili mfululizo.

Sunday, December 13, 2009

SINZA STAR YALALA TENA


Timu ya Sinza Star chini ya miaka 14 (jezi za njano) wamelala tena mbele ya watoto wenzao wa Shein Rangers bao 2 - 0, picha hii ilipigwa baada ya mchezo huo wakiwa pamoja na Shein Rangers (jezi bluu bahari).

MECHI YA WATOTO TWALIPO


Timu ya chini ya miaka 17 ya Shein Rangers Sports Club wakifatilia mechi ya wadogo zao chini ya miaka 12 mchezo uliochezwa katika uwanja wa Twalipo jijini Dar es salaam.

MAZOEZINI


Wachezaji wa timu ya watoto wa Shein Rangers Sports Club wakifatilia mazoezi ya wenzao kwa umakini.

Friday, December 11, 2009

SHEREHE ZA UHURU TANZANIA ZAFANA



Sherehe za miaka 48 ya Uhuru wa Tanganyika zilizofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar zafana. Picha ya juu ni Rais Jakaya Kikwete na mkuu majeshi ya ulinzi na usalama Jenerali Davis Mwamunyange wakati wa sherehe hizo, na picha ya chini ni kikundi cha sanaa toka Uganda kikitumbuza katika sherehe hizo.

Wednesday, December 9, 2009

MIAKA 48 YA UHURU WA TANZANIA BARA


Bodi ya Wakurugenzi, Uongozi na Wachezaji wa SHEIN RANGERS SPORTS CLUB. Wanatoa pongezi kwa Mh. Rais Jakaya Kikwete na serikali yake pamoja na watanzania wote kwa ujumla katika sherehe za kutimiza miaka 48 ya Uhuru wa Tanganyika leo tarehe 09 Desemba 2009.

SHEIN RANGERS SPORTS CLUB INAAHIDI KUSHIRIKIANA NA WANAMICHEZO WOTE ILI KULETA MAENDELEO KATIKA MICHEZO NA KUMPATIA HAKI MTOTO WA KITANZANIA KATIKA KUSHIRIKI MICHEZO.

TANZANIA BARA 4 ERITREA 0


Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania Bara mara baada ya mchezo wa robo fainali dhidi ya Eritrea, bara ili shinda bao 4 - 0 na kuingia nusu fainali.

Tuesday, December 8, 2009

TIMU YA TAIFA YA IVORY COAST KUJA TANZANIA


Timu ya Taifa ya Ivory Coast inawasili nchini tarehe 2 January 2010 kwa kambi ya wiki moja ikiwa katika maandali ya Kombe la Mataifa ya Afrika yatakayofanyika Angola, pia ikiwa Tanzania itajipima ubavu na Taifa Stars (timu ya taifa ya Tanzania) kwa michezo miwili siku ya tarehe 4 na 7 January 2010 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

MDAHALO


Siku ya terehe 10 Desemba 2009 kutakuwa na mdahalo kuhusu unyanyasaji kijinsia, mdahalo huo utafanyikia Karimjee Hall kuanzia saa nane mchana.

MADA
Je, wanaume ni chanzo cha unyanyasaji kijinsia?

MUONGOZA MADA
Jenerali Ulimwengu

Wanamichezo wote tuungane na watanzania wengine katika mapambano ya unyanyasaji kijinsia.

UJUMBE HUU UNALETWA KWENU NA:-
SHEIN RANGERS SPORTS CLUB

Monday, December 7, 2009

ZIARA YA SHEIN TWALIPO CAMP

Timu ya Shein Rangers siku ya tarehe 06 Desemba 2009 ilifanya ziara ya mafunzo katika kituo cha kukuza soka cha Twalipo Youth Soccer Foundation (TYSF) kinachomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania chini ya mwalimu wa soka Maj Bakari.

Katika ziara hiyo kulifanyika michezo ya kirafiki mitatu kwa kuzingatia umri wa wachezaji wa pande zote mbili na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:-
Mechi ya kwanza TYSF 1 - Shein Rangers 0 chini ya miaka 12
Mechi ya pili TYSF 2 - Shein Rangers 0 chini ya miaka 14
Mechi ya Tatu TYSF 1 - Shein Rangers 0 chini ya miaka 17

Uongozi wa SHEIN RANGERS SPORTS CLUB unapenda kuchukua nafasi hii kutoa shukurani kwa mapokezi mazuri na mchezo mzuri wa amani na upendo, pia tunapenda kuchua nafasi hii kutoa shukurani za dhati kwa zawadi ya mpira maalum wa kuchezea soka kwa watoto na kugharamia usafiri.

SHEIN YAFANYA ZIARA TWALIPO


Mkuu wa kituo cha kukuza soka cha Twalipo Youth Soccer Foundation (TYSF) Major Bakari kushoto katika picha ya pamoja na kocha mkuu wa Shein Rangers ndugu Rashid Said katika kituo cha soka cha Twalipo jijini Dar es Salaam, timu ya Shein ilifanya ziara ya mafunzo katika kituo hicho cha soka kwa timu zake zote tatu kupata kichapo.

MANAHODHA NA WAAMUZI


Manahodha wa timu ya (TYSF) na Shein Rangers chini ya miaka 12 wakiwa katika picha ya pamoja na waamuzi wa mchezo wao, nahodha wa Shein Rangers Moses Leonald (jezi bluu bahari) na nahodha wa (TYSF) Mussa Bakari (jezi yenye mistari ya bluu na nyekundu).

TWALIPO CHINI YA MIAKA 12


Timu ya Soka ya Kituo cha kukuza soka cha Twalipo Youth Soccer Foundation (TYSF) chini ya miaka 12.

TYSF NA SHEIN RANGERS


Timu ya Shein Rangers chini ya miaka 12 (jezi bluu bahari) na timu ya Twalipo Youth Soccer Foundation (TYSF) katika picha ya pamoja kabla ya kucheza mchezo wa kirafiki, (TYSF) ilishinda bao 1 - 0 katika mchezo uliokuwa mzuri.

MAPUMZIKO



Picha ya juu ni timu ya Shein Rangers chini ya miaka 12 na picha inayofata ni Shein chini ya miaka 17, wakati wa mapumziko katika mechi zao walizocheza na timu za kituo cha Twalipo na timu zote za Shein Rangers zili lala mbele ya vijana wa (TYSF).

NAHODHA U 12 SHEIN AMFURAHISHA MAJ BAKARI


Nahodha wa timu ya Shein Rangers chini ya miaka 12 (U12) Moses Leonald amfurahisha Maj Bakari kwa uwezo wake wa soka katika nafasi yake ya kiungo mshambuliaji.

TWALIPO WATOA ZAWADI KWA SHEIN RANGERS


Nahodha wa timu ya kituo cha kukuza soka cha Twalipo Youth Soccer Foundation (TYSF)chini ya miaka 12 (U 12) Mussa Bakari (jezi bluu bahari kushoto) akimkabidhi zawadi ya mpira maalum wa kuchezea watoto nahodha mwenzake wa timu ya watoto wa Shein Rangers Moses Leonald.

PICHA YA PAMOJA U 17


Picha ya pamoja ya Shein (chini ya miaka 17) na timu ya kituo cha kukuza soka cha Twalipo baadaya ya mchezo mkali na kuvutia kumalizika baina ya timu hizo, katika mchezo huo Twalipo ilishinda bao 1 - 0 kwa mkwaju wa penati dakika za lala salama.

DUA YA PAMOJA


Timu ya kituo cha soka ya Twalipo na Shein Rangers katika dua ya pamoja kumshukuru mungu baada ya kumaliza mchezo wao salama.

Sunday, December 6, 2009

ZUIA UKATILI KIJINSIA

SHEIN RANGERS SPORTS CLUB INAUNGANA NA KAMPENI ZA KIDUNIA YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI KIJINSIA.

NINAWAJIBIKA KWA VITENDO KATIKA FAMILIA NA JAMII YANGU.
HAUKO PEKE YAKO MWENYE NIA BINAFSI, UTHUBUTU NA UTAYARI WA KUZUIA UKATILI WA KIJINSIA.

MTANZANIA, MWANAMICHEZO ZUIA UKATILI KIJINSIA KATIKA JAMII YAKO!

Saturday, December 5, 2009

U17 SHEIN KATIKA MAANDALIZI YA MECHI NA TWALIPO



Timu ya chini ys miaka 17 ya Shein Rangers ikiwa katika maandalizi ya mchezo na timu ya kituo cha Twalipo.

SHEIN KUCHEZA NA TWALIPO

Timu za SHEIN RANGERS na KITUO CHA SOKA CHA TWALIPO kuumana katika michezo ya kirafiki siku ya tarehe 06 Desemba 2009 katika uwanja wa Twalipo jijini Dar es salaam. Mechi zinazotarajiwa kuchezwa ni tatu kwa timu chini ya miaka 12, 14 na 17. Wapenzi wa soka ya vijana wanakaribishwa kupata burudani ya soka.

SHEIN KATIKA PICHA


Picha hii ya pamoja ya timu zote tatu za SHEIN RANGERS SPORTS CLUB, chini ya miaka 17, 14 na 12.

Tuesday, December 1, 2009

SIKU YA UKIMWI DUNIA


Leo tarehe 01 Desemba 2009 ni siku ya UKIMWI duniani kote, kwa Tanzania kitaifa inafanyitika mkoani Tanga. Shein Rangers ilitumia siku hii kwa kuwakumbusha na kuwaelimisha wachezaji wake jinsi ya kujikinga na kupambana na maradhi hayo, juu pichani wachezaji wakisikiliza kwa makini.

MWENYE KIPAJI


Mtoto Semeni Sadiki ni moja kati ya watoto zaidi ya 60 walijitokeza katika usaili wa kuchezea timu ya watoto wa Shein Rangers na yeye kuwa miongoni mwa watoto wenye kipaji cha soka waliopita katika mchujo.

SEMENI MAZOEZINI



Mtoto Semeni Sadiki ambaye ana ulemavu wa ngozi akiwa na watoto wenzake(wachezaji wa shein rangers) chini ya miaka 14 katika mazoezi.

KIDUME KAZINI




Mtoto Ramadhani Kilindo maarufu kwa jina la utani "KIDUME" akiwa katika mazoezi ya shein rangers juu ni matukio tofauti ya kidume kikiwa kazini.

Monday, November 30, 2009

HENRY JOSEPH MAJUU


Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Henry Joseph Shindika anaendelea vyema kupeperusha bendera ya Tanzania na Timu yake imefanikiwa kupanda ligi kuu.

UHAI CUP 2009 YAANZA KWA KISHINDO


Mashindano ya soka kwa timu za vijana chini ya miaka 20 za ligi kuu Tanzania bara yameanza kwa kishindo baada ya timu ya Moro United kuicha JKT Ruvu ya Pwani bao 7 - 1. Timu ya vijana ya Azam ndio bingwa mtetezi.

TANZANIA YALALA 2 - 0


Tanzania bara yaanza vibaya kwa kukubali kipigo cha bao 2 - 0 toka kwa Uganda katika mashindano ya mataifa ya Afrika Mashariki na Kati maarufu kwa Chalenji Cup.

TANZANIA NA GHANA


Tanzania (Taifa Star) siku ilipokutana na Ghana katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam katika mchezo wa kirafiki mapema mwaka huu na matokeo yalikuwa 1 - 1.

TAMASHA LA WATOTO YATIMA LAFANA


Tamasha la michezo mbalimbali lililoshirikisha vituo tofauti vya watoto yatima lafana jijini Arusha, tamasha hilo liliandaliwa na wafanyakazi wa Vodacom Arusha.

PONGEZI KWA HADIJA MALOYA


Uongozi wa timu ya SHEIN RANGERS SPORTS CLUB unatoa pongezi kwa dada yetu Hadija Maloya kwa kuifatilia blog hii kwa karibu pamoja na kutoa ushauri na comment kila mara anajulikana zaidi kwa jina la "MKWE"

WAKUSHI WALALA KWA SINZA STARS

Timu ya Wakushi FC ya Sinza Palestina imekubali kipigo cha bao 1 - 0 toka kwa sinza stars katika mchezo wa ligi ya TFF wilaya ya Kinondoni siku ya tarehe 29 Novemba 2009 katika uwanja wa Kinesi jijini Dar es salaam.

IDD AL HAJI

Timu ya Shein Rangers wakati wote wa sikukuu ya iddi al haji ilitoa mapumziko kwa wachezaji wake, hakukua na mechi wala mazoezi na tunashukuru mungu mazoezi yameanza leo tarehe 30 Novemba 2009 wachezaji na viongozi wote wapo salama.

Monday, November 23, 2009

JUHUDI FC YAVUNJA MWIKO WA SHEIN

JUMAPILI TEREHE 22 NOVEMBA 2009
Timu ya Shein Rangers imepoteza mchezo wa pili toka mwaka huu uanze na mchezo wa kwanza kupoteza nyumbani toka mwaka huu uanze. Timu ya Shein Rangers ilicheza mchezo wa kirafiki na timu ya Juhudi FC na kufungwa 3 - 2 katika uwanja wake wa nyumbani.
Juhudi FC ndio timu ya kwanza kuifunga Shein Rangers nyumbani mwaka huu 2009.

JUMAMOSI TAREHE 21 NOVEMBA 2009
Timu ya Shein ilicheza na Vijana ya Tandika na Shein ilishinda 4 - 1 katika uwanja wa T.P Afrika Sinza.

IJUMAA TEREHE 20 NOVEMBA 2009
Shein ilikuwa icheze mechi ya ligi ya KANUNI CUP na Sinza Stars, sinza star hawakutokea uwanjani na shein kupata point tatu za chee na mabao mawili.
Hata hivyo shein ilicheza mchezo wa kirafiki na Wazwazwa ya Mburahati na shein kushinda bao 2 - 1.

Friday, November 20, 2009

KOMBE LA DUNIA LATUA TENA TANZANIA



Kombe la FIFA la Soka la Dunia limetua nchini Tanzania kwa mara ya pili katika historia yake hapa duniani,juu ni picha tofauti za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete alipolizindua katika uwanja mpya wa Taifa na pia alitumia nafasi hiyo kuwafumbua macho viongozi wa TFF kuacha kukombatia timu kubwa na badala yake kuwekeza katika soka la vijana na watoto.

TWALIPO YOUTH SOCCER FOUNDATION (TYSF) NDANI YA TOVUTI


Hizi ni picha tofauti za watoto wa Kituo cha kukuza soka cha TWALIPO YOUTH SOCCER FOUNDATION cha Jijini Dar es salaam kinachomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania. Chini ya mwalimu wa soka Maj Bakari.Kituo hicho kimetengeneza tovuti yake kwa habari zaidi tembelea www.twalipoyouthsoccerfoundation.com

Thursday, November 19, 2009

MWALIMU NA VIFAA


Kocha mkuu wa Shein Rangers Rashid Said akiwa katika moja ya maduka ya vifaa vya michezo alipoenda kuchukua vifaa vya michezo.

WALIOPITA USAILI SHEIN WAANZA MAZOEZI


Wachezaji wa umri chini ya miaka 14 waliopita katika usaili wa timu ya Shein Rangers Sports Club wameanza rasmi mazoezi kwa ajili ya kutengeneza timu mpya ya watoto.

Wednesday, November 18, 2009

Player Information For MURSHID ALLY RASHID

Personal Details
Full name Murshid Ally Rashid
Age17 years old
Membership ID46852
Location Yorkshire
Nationality Tanzanian
Current level Semi pro
Wants trials at Premiership

Physical Attributes
Dominant foot Both
Height5' 6''
Weight10 st 1 lbs
Speed More Quick

Preferred Positions
Forward/Left winger/Right winger

Career To Date
I learned to play football in the street in Tanzania aged seven . When Iwas 14 i joined Shein Rangers Sports Club (check on www.sheinrangers.blogspot.com), in Dar es salaam and between 2006 and 2009 I palyed in 109 games, scoring 74 goals. I was selected to play at district and regional levels, then i joined the Tanzania Natonal football team and I have played 13 friendly match and 6 league with Malawi,Nigeria , Kenya, Namibia, Ethopia and Africa Invatations team,in June 2009 I was Selected to play in the Copa Coca Cola intarnational tournarment in South Africa and as a result iwas chosen be one of the eight highly ranked under 17 players in Africa. Our National team got a 3rd place. Right now I am playing for Azam football club in Dar es Salaam.

Trials To Date
I have taken part in five Trials in Tanzania for Shein Rangers Sports Club, the districkt and regional teams,Azam football Club and U 17 National team. I hope to attend my first Trial in the uk, in December

How To Contact This Player
Click here to contact this player via www.footballcv.com

TAARIFA HIZI ZIMENASWA NA BLOG HII TOKA MTANDAO WA www.fooballcv.com WA UINGELEZA.

SHEIN RANGERS YAANZA KWA SALE

Timu ya Shein Rangers imeanza kwa sale ya bila kufungana na timu ya Eagle Fry ya Mburahati katika mchezo mgumu wa mashindano ya KANUNI CUP 2009. Mchezo huo ulichezwa tarehe 16 Novemba 2009 katika uwanja wa Bubu Mburahati, shein itajitupa tena uwanjani tarehe 20 Novemba 2009 na Sinza Star katika uwanja huo huo.

Taarifa hizi na:-
Rashid Said (Kocha mkuu Shein Rangers Sports Club)

ABAJALO YAJITOA LIGI YA TFF

Timu ya soka ya Abajalo ya Sinza imejitoa katika mashindano ya ligi ya TFF Wilaya ya Kinondoni, kujitoa kwao kuizawadia point tatu za chee mahasimu wao Sinza Stars na kushika nafasi ya pili katika kundi lao.

Monday, November 16, 2009

KANUNI CUP 2009

Uongozi wa mashindano ya KANUNI CUP 2009 umeiomba radhi timu ya Shein Rangers kwa kitendo cha kuwakataa baadhi ya wachezaji wao na kuiomba ishiriki mashindano yao kama awali bila ya masharti yoyote.

SHEIN RANGERS UFUKWENI


Timu ya Shein Rangers ilipokuwa mapumzikoni katika pwani ya bahari ya hindi mapema mwaka huu.

KUTANA NA "KIDUME" SHEIN RANGERS



Mtoto Ramadhani Kilindo mwenye umri wa miaka 6 amekuwa kivutio katika mazoezi ya timu ya watoto chini ya miaka 14 ya Shein Rangers,Ramadhani maarufu kwa jina la " Kidume" katika picha zake tofauti akiwa mazoezini, moja ya sifa zake ni mbio na kutokata tamaa na kila jambo anata kujaribu na kuweza. Mambo yake ni kivutio tosha mazoezini, huyo ndio KIDUME kama wenzake wanavyomwita.

SHEIN MAZOEZINI


Timu ya Shein Rangers ikiwa katika mazoezi yake ya kawaida katika uwanja wa TP Sinza.

Wednesday, November 11, 2009

MAZOEZI YAENDELEA SHEIN RANGERS

Timu ya Shein Rangers baada ya kujitoa katika mashindano ya KANUNI CUP 2009 kutokana na mizengwe, inaendelea na mazoezi yake ya kawaida kila siku jioni katika uwanja wa T.P. Africa Sinza.

Taarifa hii kutoka Uongozi wa Shein Rangers Sports Club.